,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Thursday, March 23, 2017


Jeshi la polisi nchini Uingereza limesema kwamba mwanaume aliyehusika katika shambulio la kigaidi katika eneo la Westminister kuwa ni Khalid Masood, kwa mujibu wa taarifa walizopewa na wapelelezi wa Scotland Yard.

Wapelelezi hao wamesema kwamba Masood anaekadiriwa kuwa na umri wa miaka 52 alizaliwa katika eneo la Kent na wapelelezi wanaamini kwamba alikuwa akiishi Midlands magharibi.

Hatahivyo, alitambuliwa na polisi na kwamba alikuwa ameshtakiwa kwa kushambulia watu ikiwemo umiliki wa silaha na kusababisha taharuki mbele ya uma.


Watu saba wamekamatwa katika uvamizi mjini London na Birminghamkufuatia shambulio la Westminster lililowauwa watu wanne, kwa mujibu wa polisi. 

Mamia ya polisi wa upelelelezi wamekuwa wakifanya kazi usiku kucha wakifanya uchunguzi dhidi ya makazi sita, amesema kaimu naibu wa kamishna wa polisi Mark Rowley.

Wale waliokufa walikuwa ni mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 40, mwanamume mwenye miaka 50 Polisi Keith Palmer pamoja na mshambuliaji, aliongeza.

Saba miongoni mwa majeruhi bado wako hospitalini katika hali mahututi.

Wengine 29 zaidi wamekuwa wakipata matibabu hospitalini, ameongeza Rowley.

Katika shambulio la Jumatano, mwanamume mmoja aliendesha gari kwenye njia ndogo karibu na Westminster na kuwagonga wapitanjia, huku akiwaacha kadhaa na majeruhi.
Kisha alimdunga kisu polisi na akapigwa risasi na polisi kwenye eneo la bunge.

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi