,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Thursday, March 23, 2017

Wanandinga wanaounda kikosi cha Serengeti Boys wamekabidhiwa kadi zao za bima ya afya toka katika mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF katika makao makuu ya mfuko huo yaliyopo kurasini jijini dar es Salaam.

Akiwakabidhi kadi hizo kwa wanandinga hao, Kaimu Mkurugenzi wa Masoko NHIF Bi Angela Mzirai amesema kutokana na dhoruba ambazo zimekuwa zikiwakuta wanamichezo wawapo uwanjani ni vema wanamichezo wakawa na bima ya afya kwani maradhi au majeraha hujitokeza muda wowote ule.
Angela amesema NHIF wamefikia katika hatua ya kuwasajili wanandinga wa Serengeti katika mfuko huo kwani NHIF inthamini sana michezo na pia mfuko huo umetoa fursa kwa wanandiga hao kutumia chumba cha kufanyia mazoezi kilichopo katika ofisi za mfuko huo.

Katika hatua nyingine Angela ameipongeza Serengeti Boys kwa kufanikiwa kupata nafasi ya kwenda kushiriki katika fainali za AFCON kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 zinazotaraji kwenda kufanyika nchini Gabon.


Angela amesema Serengeti imepiga hatua kubwa katika maendeleo ya mchezo wa soka nchini kwani sasa inaliwakilisha vema Taifa na kulitangaza kimataifa.

Nae Meneja Wanachama wa NHIF Elentruda Mbogoro amewataka wanamichezo katika mbalimbali kujiandikisha katika mfuko huo kuanzia ngazi ya michezo ya mashule hadi katika ligi mbali mbali.

Wakati huo huo Katibu Mkuu wa TFF Mwesigwa Selestine ameishukuru NHIF kwa kuwapatia wanandinga hao kadi hizo.
-

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi