,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Wednesday, April 15, 2015



Serikali ya Kenya imeahidi kuwasamehe wakenya ambao wamepokea mafunzo ya kigaidi endapo watajitokeza katika kipindi cha siku 10 zijazo.


Waziri wa usalama wa ndani jenerali mstaafu Joseph Nkaissery pia amewaonya wazazi wa vijana kama hao kwamba watachukuliwa hatua kali endapo hawataijulisha serikali kuhusu kujiunga kwa wanao na kundi la Al Shabaab.

Serikali imewapa wale wote waliopokea mafunzo kutoka kwa Al Shabaab siku kumi kupiga ripoti kwa afisi za wasimamizi wa miji ya Garissa, Mombasa ama Nairobi.
Waziri huyo wa usalama pia amechapisha nambari za simu ambazo vijana hao wanaweza kutumia kutoa ripoti hizo kisiri.
Amesema wale watakaoitikia mwito wake watasamehewa na kupata usaidizi wa kurejea katika jamii.

Hata hivyo amewaonya wale ambao hawatafanya hivyo katika siku kumi zijazo kwamba serikali itakabiliana nao kama wahalifu kwa mujibu wa sheria za Kenya.

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi