Serikali ya Kenya imeahidi
kuwasamehe wakenya ambao wamepokea mafunzo ya kigaidi endapo
watajitokeza katika kipindi cha siku 10 zijazo.
Serikali imewapa wale wote waliopokea mafunzo kutoka kwa Al Shabaab siku kumi kupiga ripoti kwa afisi za wasimamizi wa miji ya Garissa, Mombasa ama Nairobi.
Amesema wale watakaoitikia mwito wake watasamehewa na kupata usaidizi wa kurejea katika jamii.
Hata hivyo amewaonya wale ambao hawatafanya hivyo katika siku kumi zijazo kwamba serikali itakabiliana nao kama wahalifu kwa mujibu wa sheria za Kenya.

0 comments:
Post a Comment