Wasanii mbalimbali wanaochipukia katika sanaa ya uigizaji nchini wamejitokeza katika usaili uliofanyika katika kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam kutafuta fursa ya kushiriki katika Tamthilia ya WHO CHEAT.
Blogu ya Jamii
imeshuhudia mamia ya wasanii waliojitokeza kushiriki katika usaili huo
ulioandaliwa na Ndauka Advert kwa ushirikiano na Afrika Swahili TV.
Katika Usaili huo
msanii na muigizaji wa filamu nchini Rose Ndauka amesema amefurahishwa na
kuridhishwa na vipaji vilivyojitokeza.
Ndauka amesema
wasanii waliojitokeza wameonyesha vipaji vya hali ya juu hivyo anaamini atapata
waigizaji wazuri na watakaoleta chachu katika tamthilia hiyo.
Nao baadhi ya wasanii
waliojitokeza ili kuwania nafasi ya kushiriki katika tamthilia hiyo wameahidi
kuhakikisha wanatumia vema fursa iliyojitokeza ili waweze kuleta mawazo mapya
katika tasnia ya uigizaji nchini.







0 comments:
Post a Comment