,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Wednesday, April 15, 2015



Kwa mara nyingine tena, Uchina imemlaumu kiongozi wa Tibet aliyeko uhamishoni Dalai Lama, kwa kutokuwa mwaaminifu na kushinikiza kiujanja uhuru wa watu wa Tibet.


China inadai kuwa kiongozi huyo amebadilisha mbinu badala ya kutaka kutambuliwa kwa jimbo hilo kama alivyokuwa akishinikiza hapo awali.

China imeanzisha makabiliano makali dhidi ya kiongozi wa kidini wa watu wa Tibet, Dalai Lama, na kumlaumu kwa kutumia ghasia kushunikiza uhuru wa Tibet.
 
Katika taarifa ndefu inayoelezea mfumo mzima ya maoni ya jimbo la Himalaya, China inasema kuwa katika hali ilivyo sasa, hakuna haja kabisa ya kufanya mazungumzo na kinara huyo wa kidini aliye uhamishoni India.

Kwa muda mrefu Dalai Lama amekuwa akitetea uhuru wa kujitenga wa jimbo la Tibet, na alikuwa na matumaini makubwa kwa Rais wa sasa wa China, Xi Jinping, atatumia mbinu tofauti katika uhusiano naye na wa watu wa Tibet.

Taarifa hiyo pia ambayo ilichapishwa na shirika la habari la kitaifa la Xinhua, inasema kuwa wakuu mjini Beijing wanamuomba Dalai Lama kuweka kando ndoto yake ya hatma ya baadaye ya Tibet.

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi