Katibu mkuu wa klabu ya Yanga Charles Boniface Mkwasa amekiri kwamba klabu hiyo inadaiwa na aliekuwa kocha wa klabu hiyo na baadae kuwa Mkurugenzi wa Ufundi, Hans va der Pluilm raia wa Uholanzi.
Katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
Mkwasa amesema uongozi wa klabu ya yanga unasubiri Hans awasilishe kiiasi cha
fedha ambacho anaidai klabu ya Yanga ili klabu hiyo iweze kumlipa fedha zake.
Mkwasa amesema Yanga imepita katika mchakato wa kupunguza
baadhi ya watu waliokuwa wakihudumu katika klabu hiyo kama sehemu ya kubana
matumizi kama ambavyo makampuni mengi hufanya, lakini hilo halimaanishi kwamba
klabu hiyo ina ukata wa fedha.
Katika hatua nyingine
Kocha Msaidizi wa klabu ya Yanga mwalimu Juma Mwambusi amesema kikosi chake
kipo katika hari ya kupata matokeo katika mchezo wa siku ya jumamosi dhidi ya
zanaco katika ligi ya mabingwa barani Afrika hatua ya mtoano.
Kocha Mwambusi amesema
kikosi chake kinakabiliwa na baadhi ya wanandinga ambao wanaweza kuukosa mchezo
wa siku ya Jumamosi utakaopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
lakini hana shaka na ushindi kwani ana kikosi kikubwa.

0 comments:
Post a Comment