Tanzania imepanda kwa nafasi moja katika
viwango vipya vya soka vilivyochapishwa na Shiirikisho la mchezo wa soka
duniani FIFA na sasa kufikia nafasi ya 157 mara baada ya kukusanya alama 157, ikiwa ni ongezeko la
alama 5 kwani katika viwango vilivyopita ilikuwa na
alama 152 na kkushika nafasi ya 158 kwa ubora duniani.
Afisa Habari wa klabu ya TFF Alfred Lucas amesema
ili Tanzania iweze kupanda zaidi katika viwango vya soka duniani ni lazima
michezo mbalimbali ya kimataifa ipatikane.
Kwa upande wa mataifa mengine yaliyopo katika
ukanda wa Afrika Mashariki Uganda inaendelea kushika usukani katika ukanda huo
ikiwa inashikilia nafasi ya 74 duniani, na kwa upande wa bara la Afrika
inashika nafasi ya 16.
Kenya inashika nafasi ya ya 21 kwa bara la
Afrika na nafasi ya 88 duniani wakati Rwanda inashika nafasi ya 24 Afrika na 93.
Burundi inashika nafasi ya 41 Afrika na 139
duniani.
Wakati huo
huo Misri imeendelea kuwa kinara kwa kukwea kwa nafasi mbili zaidi hadi nafasi
ya 20 kwa ubora duniani, ikifuatiwa na Senegal iliyopo nafasi ya 28 huku
mabingwa wa michuano ya Mataifa ya Afrika Cameroon nao wakikwea kwa nafasi moja
hadi nafasi ya 32 duniani.
Kwa upande
wa mashirikisho yote ya soka pamoja na vyama duniani, Argentina imeendeleza
kushika usukani kwa kumata nafasi ya kwanza, nafasi ya pili imekwwenda kwa
Brazil, na nafasi ya tatu imekwenda kwa Ujerumani na nafasi ya tatu imeshikwa
na Chile.
Mataifa mengine yenye nguvu katika mchezo wa
soka pamoja na nafasi wanazoshika, Ufaransa inashika nafasi ya saba, Hispania kumi,
na Uingereza nafasi ya 14.
0 comments:
Post a Comment