MTOTO wa staa wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel, Cookie amegeuka kivutio baada ya kufikishwa kwenye Shule ya LJAY BUSY BEES iliyopo maeneo ya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar.
Cookie mwenye umri wa mwaka mmoja na siku 30 amefikishwa kwenye shule hiyo hivi karibuni kuanza masomo yake ambapo siku ya kwanza akiwa na mama yake aligeuka kivutio kwa walimu na wanafunzi wenzake huku akionekana mwenye uelewa mkubwa wa mambo.
“Cookie tumeona akulie kwenye mazingira ya shule, tumekubaliana na baba yake (Moze Iyobo) aanze shule tukiamini itakuwa na faida. Ana umri mdogo lakini anaonekana kuwa na uelewa mkubwa wa mambo hadi walimu wanamshangaa. Mungu amsaidie kwenye masomo yake,” alisema Aunt.
0 comments:
Post a Comment