Msanii
wa kike wa Bongo Fleva ambaye kwa sasa anasumbua na wimbo wake wa One
More Night, Hadija Maige ‘Kadja Nito’ anadaiwa kupigwa ndoa ya fasta
siku chache baada ya Mfungo wa Ramadhani kuanza.
Chanzo
ambacho ni rafiki wa msanii huyo kilitung’ata sikio kuwa, Kadja ambaye
ni mama wa mtoto mmoja alikuwa na jamaa yake ambaye alimuomba amuoe
kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili akampikie futari, mambo
yakaenda sawa na ndoa ikafungwa kimyakimya.
Baada
ya kunasa ubuyu huo, paparazi wetu alimvutia waya Kadja na kumuuliza
kuhusu jambo hilo la heri ambapo alifunguka: “Mmh! Yaani ninyi bwana,
mimi siyo wa kuolewa ndoa ya futari, halafu nachukia sana kufuatiliwa
mambo yangu binafsi.
“Mambo ya ndoa sasa hivi yanakujaje, wewe niulize nina wimbo gani mpya, naendeleaje na swaumu, hapo sawa.”
0 comments:
Post a Comment