Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewaagiza
watumishi wa wizara hiyo katika kitengo cha huduma kwa wateja, kufanya
kazi hadi usiku ili
kuhakikisha wanawahudumia kwa muda wananchi wengi
wanaofika katika kitengo hicho na kuondoka bila kupata huduma stahiki.
Waziri
Lukuvi alitoa maagizo hayo jana alipofanya ziara katika kitengo hicho
na kubaini kuwepo urasimu mkubwa unaopelekea wananchi kushindwa kupata
huduma kwa wakati.
Baada ya kuzungumza na baadhi ya wananchi waliofika katika kitengo hicho, alibaini kuwepo wananchi ambao wamekuwa wakifuatilia hati zao kwa takribani miezi mitatu bila mafanikio lakini alipoagiza wapewe hati hizo zilipatikana mara moja.
Baada ya kuzungumza na baadhi ya wananchi waliofika katika kitengo hicho, alibaini kuwepo wananchi ambao wamekuwa wakifuatilia hati zao kwa takribani miezi mitatu bila mafanikio lakini alipoagiza wapewe hati hizo zilipatikana mara moja.
“Watu
wasirudi bila kuhudumiwa. Na kama ni wafanyakazi watabaki mpaka usiku,
tutafanya utaratibu wa hao wafanyakazi wanaobaki mpaka usiku.
Wafanyakazi wabaki muda zaidi lakini kila anayekuja katika kituo kile
lazima ahudumiwe,” alisema Lukuvi.
0 comments:
Post a Comment