,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Wednesday, August 28, 2013

PictureMansour Yussuf Himid
Mansour anaelezwa kuwa ni shemeji yake na Rais Mstaafu Amani Abeid Karume.

Mansour aliteuliwa kuwa mjumbe wa baraza la wawakilishi na Rais Karume mwaka 2000 na kuteuliwa kushika wadhifa wa Naibu Waziri wa Maji, Nishati Ujenzi na Ardhi hadi mwaka 2005.

Mwaka 2005 alichaguliwa kuwa Mwakilishi wa Kiembe Samaki kupitia CCM, nafasi ambayo amedumu nayo hadi sasa. Mwaka huo aliteuliwa na Rais Karume kuwa Waziri wa Maji, Nishati Ujenzi na Ardhi hadi mwaka 2010.

Kati ya 2005 -2010 alikuwa Mweka Hazina wa CCM Zanzibar  wadhifa ulimpa fursa ya kuwa Mjumbe wa NEC na Kamati Kuu ya CCM. Mwaka 2010 hadi mwaka 2012, alikuwa Waziri wa Kilimo na Rasilimali.

Ilipofika 2009 alikuwa mstari wa mbele kuushutumu Muungano kuwa ni chanzo cha kudorora kwa Zanzibar huku akiendesha kampeni juu ya suala la mafuta kutokuwa la Muungano.

Katika uchaguzi wa mwaka jana ndani ya CCM, Mansour hakugombea nafasi yoyote ndani ya CCM.

Aidha, alihudumu kama mjumbe wa Baraza la Biashara la Zanzibar kati ya mwaka 2002 hadi 2012.

Kutokana na misimamo yake ndani na nje ya chama na Serikali, Oktoba 15, 2012, Dk. Shein ilifuta uteuzi wa

Mansour kama waziri hivyo kubakia kuwa mjumbe wa Baraza la Wawakilishi hadi Agosti 26, 2013.

Mansour ni mwanasiasa na mfanyabiashara aliyezaliwa Novemba 3, 1967 kisiwani Unguja. Alisoma masomo yake ya msingi na sekondari nchini India kati ya mwaka 1976 na 1987.

Kabla ya kuingia rasmi katika siasa mwaka 2000, aliteuliwa kuwa mjumbe katika Baraza la Wawakilishi na alijihusisha katika biashara ya hoteli.

Mwanasiasa huyo ni mtoto wa Mkuu wa Kwanza wa Jeshi la Zanzibar baada ya Mapinduzi, Brigedia Jenerali Yussuf Himid.

Amekuwa akisimamia maridhiano ya Wazanzibari na Umoja wa Kitaifa akiwa mmoja wa wajumbe sita wa Kamati ya Maridhiano aliyoshiriki kikamilifu kuyaanzisha mwaka 2009.

Pia ni miongoni mwa Wazanzibari walio mstari wa mbele kutetea muundo wa Muungano, utakaoipa Zanzibar mamlaka kamili ya dola.

Wajumbe wengine wa Kamati hiyo ni Mwenyekiti Hassan Nassor Moyo (CCM), Eddie Riyami (CCM), Abubakar Khamis Bakari (CUF), Ismail Jussa Ladhu (CUF) na Salim Bimani (CUF).

Katika hatua nyingine Nec iliyokaa kwa siku tatu mjini Dodoma chini ya mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, pia kimeridhia uteuzi wa makatibu wa wapya wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Jumuiya ya Wazazi na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).

Katika uteuzi huo aliyekuwa Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro, Sixtus Mapunda, ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, nafasi  iliyokuwa ikishikiliwa na Shigela.

Taarifa za zaidi kutoka Dodoma ambazo zimelifikia gazeti hili jana jioni, zinasema kwamba Seif Shabani Mohamed ambaye ni mjumbe wa NEC kutoka Pemba ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Hamis Suleiman Dadi huku Amina Makilagi akiachwa kuendelea na nafasi yake ya Katibu Mkuu UWT.

Pia, NEC imeridhia mapendekezo ya CC ya kuziba nafasi za Makatibu wa CCM wa mikoa ya Morogoro, Kaskazini Pemba na Geita ambayo yamekuwa wazi kwa muda mrefu sasa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo.
Kutokana na hali hiyo, Romuli Rojas John ameteuliwa kuwa Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro. John kabla ya uteuzi huo alikuwa Msaidizi Kitengo cha Uchaguzi, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM.
Aidha, Katibu wa CCM wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, Kassim Mabrouk Mbarak, ameteuliwa kuwa Katibu mkoa Kaskazini Pemba wakati aliyekuwa Katibu wa CCM Wilaya ya Igunga ameteuliwa kuwa Katibu wa CCM mkoa wa Geita.
---Maelezo haya ni kwa mujibu wa sehemu ya taarifa iliyochapishwa kwenye gazeti la NIPASHE

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi