Unakumbuka zile habari za Wema Isaac
Sepetu kununuliwa jumba la kifahari na bilionea mmoja Kijitonyama, Dar?
Sasa zimegeukia kwa staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ambaye
naye kuna madai mazito ya kuhongwa nyumba.
Ilikuwa mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo gazeti hili lilipokea ujumbe mfupi wa simu ya mkononi ‘sms’ kutoka kwa chanzo chake.
Chanzo: Hivi ninyi mna habari?
Risasi Jumamosi: Nyingi tu lakini kama una ya kwako itatufaa sana.
Chanzo: Kwa taarifa yenu Nisha
kanunuliwa bonge la mjengo hapa Kijitonyama karibu kabisa na Kituo cha
Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’.
Risasi Jumamosi: Nani kamnunulia?
Chanzo: Nasikia ni bilionea mmoja mwenye fedha zake hapa Dar es Salaam, kainunua kisha kamhonga Nisha kwa sababu ni mpenzi wake.
Risasi Jumamosi: Tunashukuru kwa taarifa, kaa mkao wa kula itaruka hewani mara moja baada ya upelelezi wetu.
RISASI LATUA KIJITONYAMA
Baada ya kuzinyaka habari hizo,
gazeti hili lilisaga soli hadi maeneo hayo na kuanza kugonga geti moja
baada ya lingine hadi lilipofanikiwa kuinasa nyumba hiyo huku Nisha
akiwa ndani kapumzika.
Msichana aliyejitambulisha kuwa ni
dada wa kazi au hausigeli kwa lugha laini ndiye aliyetoboa siri kuwa ni
kweli staa huyo yupo ndani na amehamia mahali hapo muda si mrefu.
RISASI LAINGIA MJENGONI
Risasi Jumamosi liliomba kukaribishwa
ndani ili kupata ‘ditelzi’ na ndipo Nisha akaamka na kuamua kuacha
paparazi wetu apige picha japo awali alitia ngumu akidai hayuko tayari
kuianika nyumba hiyo.
Ndani ya nyumba hiyo yenye vyumba
vitano, sebule, jiko, choo na mabafu mawili, anayeishi Nisha na dada
wake wa kazi, kuna samani nyingi za bei mbaya, mazagazaga kibao, mazulia
na marumaru huku kila kona kukiwa na Tv ya flat screen hadi chooni
(angalia picha Uk.1).
NISHA ABANWA KUHUSU UMILIKI
Nisha anayemiliki kampuni ya
kuzalisha muvi za Kibongo ya Nisha’s Film Production alipotakiwa kueleza
kama kanunua, kanunuliwa au kapangisha nyumba hiyo, alikuwa na haya ya
kusema:
“Ni juhudi zangu binafsi jamani,
kujituma sana kwenye kazi yangu ya filamu. Kuhusu kununua au kupangisha
naomba nikimaliza ‘process’ f’lanif’lani ndipo nitaweka wazi, kwa sasa
bado ni mapema mno.”
Risasi Jumamosi: Kuna madai kuwa umehongwa hii nyumba na bilionea mmoja wa hapa Dar, je, ni kweli?
Nisha: Hakuna kitu kama hicho jamani,
hayo ni maneno ya watu wasiojituma kufanya kazi kwa bidii. Haya ni
matunda ya kufanya kazi sana.
Risasi Jumamosi: Nyumba hii ina samani mpya zote za thamani kubwa sana, je, zimegharimu fedha kiasi gani?
Nisha: Vitu vyote vya ndani hadi
nikahamia vimegharimu karibu Sh. milioni 95. Ni fedha zilizotokana na
mauzo ya filamu zangu nne nilizotengeneza mwenyewe mwaka jana.
Risasi Jumamosi: Kuna madai kuwa umejiunga Freemason ndiyo maana ndani ya kipindi kifupi mambo yako safi, je, ni kweli?
Nisha: Nimesikia hizo tetesi za
Freemason ‘but’ naamini mti wenye matunda ndiyo hupigwa mawe. Mimi
namwachia Mungu, namuomba kila siku anipe baraka zake, namshukuru na
nazidi kumuomba nifanikiwe
0 comments:
Post a Comment