,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Thursday, March 9, 2017


Mkurugenzi mkuu wa Wakala wa wa kupiga vita dawa zilizokatazwa michezoni Wada, Olivier Niggli amesema haridhishwi na jitihada ambazo zimekuwa zikifanywa na Urusi katika upigaji vita wa dawa zilizokatazwa michezoni.

Takwimu zilizotolewa na WADA zilionesha kwamba zaidi ywa wanamichezo 1,000 walinufaika kwa namna moja au nyingine kutokana na matumizi ya dawa zilizokatazwa michezoni kti ya mwaka 2011 - 2015.
Kutokana na tatizo hilo kuonekana kuwa kubwa nchini Urusi viongozi  wa michezo mbalimbali nchini humo wameahidi kupigana katika vita hiyo dhidi ya dawa zilizopigwa marufuku michezoni.
Ngili amesema jitihada zinazofanywa na Urusi ni ndogo na haziendani kabisa na kasi ya upigaji vita wa dawa za kusisimua misuli ndio sababu wanamichezo mbalimbali wa Urusi wamepigwa marufuku ya kushiriki katika michezo mbalimbali.
Miongoni mwa wanamichezo hao ni pamoja na wanariadha ambao wamepigwa marufuku na Chama cha Mchezo wa Riadha duniani IAAF
Kuhusu mchakato wa ushiriki wa Urusi kupewa nafasi ya kushiriki katika michezo ya Olimpiki ya majira ya joto mwakani Katibu huyo amesema watatazama kama hilo litawezekana, lakini kubwa ni kwamba litategemea na jitihada watakazozionyesha katika upigaji vita wa dawa za kusisimua misuli.

Wakati huo huo Urusi imeandaa mpango wa kuweka mabango pembezoni mwa barabara kama sehemu ya kuonyesha hisia zake juu ya upigaji vita dawa hizo.

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi