,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Thursday, March 23, 2017



Majiji ya Paris na Los Angeles yameonyesha nia ya kuandaa michuano ya Olympics pamoja na michuano ya wachezaji wenye ulemavu ya Paralympics ya mwaka 2024 na sio michuano ya 2028.

Hata hivyo kamati ya kimataifa ya Olimpiki imeonyesha nia ya kuipa miji hiyo nafasi ya kuandaa michuano ya olimpiki ya mwaka 2024 na 2028 mwezi September.


Mpiga makasi wa Ufaransa Tony Estanguet amesema wakati sahihi kwa jiji la paris kuandaa fainali hizo ni mwaka 2024 na kama hilo litashindikana anaona itakuwa sio rahisi kwa jiji hilo kuandaa tena fainali za michuano ya olimpiki.

Tony Estanguet amesema kuandaa michuano hiyo kwa mwaka 2024 itakuwa ni rahisi kwani miundo mbinu iliyopo inaweza kutumika lakini jiji hilo halina fungu kwaajili ya kuandaa michuano hiyo mwaka 2028.


Sababu hasa ya jiji la paris kutaka kuhodhi michuano hiyo kwa mwka a2024 ni kwasababu serikali ya nchi hiyo ipo tayari kutoa ushirikiano kwa asilimia 95%.

Kwa upande wa kamati ya olimpiki ya jiji la Las Angels imejipigia chapuo kwa kusema kwamba michuano hiyo ikifanyika katika jiji hilo itakuwa imefanyika katika jiji sahihi kwa muda sahihi.

Maandalizi katika jiji hilo yako tayari kwa asilimia 88% kwani miundombinu itakayotumika ni miundombinu ya uma huku swala la usalama nalo likichukua nafasi kubwa.

Hata hivyo kumekuwepo na taarifa zinazosema kwamba jiji litakalokosa nafasi ya kuandaa michuano hiyo mwaka 2024 litapewa fursa ya kuandaa fainali hizo mwaka 2028.

Kura ya nani atakayepata fursa ya kuandaa michuano ya mwkaa 2024 inataraji kuamuliwa na wajumbe wa kamati ya kimataifa ya Olimpiki IOC.

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi