Klabu
ya Azam FC imekamilisha maandalizi yote kuelekea katika mchezo wao wa siku ya
Jumapili dhidi ya klabu ya Mbabane Swallows katika mchezo utakaopigwa katika
uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi.
Akizungumzia
maandalizi ya Azam Afisa Habari wa Azam FC Japhary Iddi Maganga amesema tayari
maandalizi ya awali yameshakamilika na kikosi cha klabu hiyo kilichopo chini ya
kocha Aristica Cioaba kipo katika hari ya juu ya kutafuta matokeo katika mchezo
wao wa awali.
Japha
amesema mchezo huo utapigwa majira ya saa moja na robo usiku ili kutoa fursa
kwa watanzania wengi kujitokeza kushuhudia mchezo huo, huku akiwataka wapenzi
na wadau wa soka wakate tiketi mapema kuepuka usumbufu kwani uwanja wa Azam
Complex una uwezo wa kuchukua mashabiki 700 tu.
Katika
hatua nyingine Japha amewataka watanzania wajitokeze kwa wingi pia katika
mchezo unaoikutanisha klabu ya Yanga dhidi ya Zanaco kwani ushindi wa Yanga ni
ushindi wa watanzania.
0 comments:
Post a Comment