Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Bw. Yusuph Manji ameikabidhi Yanga eneo la ekari 715 lililopo maeneo ya Gezaulole, Kigamboni kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa kisasa wa klabu hiyo pamoja na kituo maalum cha kukuza vipaji vya michezo.
Wasaidizi wa Manji walikabidhi eneo hilo kwa Mwenyekiti wa Baraza la wadhamini wa klabu hiyo mama Fatma Karume katika hafla fupi ambayo pia ilihudhuriwa na Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba.
0 comments:
Post a Comment