Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla leo amewatembelea wananchi wa kitongoji cha Kibundungulu kijiji cha Mbaka wilayani Rungwe ambao tangu mwezi januari mwaka huu wamekuwa wakipata tabu kupata huduma za jamii ikiwemo afya elimu na masoko kutokana na kukosa kivuko baada kivuko cha awali kusombwa na mafuriko
Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi katika kipindi hiki kuacha kuvuka kwa kutumia waya zilizofungwa kwasasa na anaamini kujengwa kwa kivuko hiki kinawasaidia wananchi kuvuka hata kipindi cha mvua nyingi
Hatua za kujenga kivuko hiki ni za dharura na muda mfupi na serikali itaweka katika mipango ili kujenga daraja la kudumu 







0 comments:
Post a Comment