Mchumba wa Mabeste, Lisa Fickenscher amesema kuwa kwa sasa hatasimamia mtu mmoja na badala yake atafanya project zitakazosaidia watu wengi kwenye jamii.
Lisa kwa sasa anasimamia kazi za mtoto wake [Kendrick] pia aliwahi kumsimamia mtoto wa H Baba na Flora Mvungi, Tanzanite.
Akiongea na Bongo5, Lisa amesema kwa sasa anataka kujihusisha kwenye kazi za kusaidia jamii na siyo kusimamia mtu mmoja mmoja.
“Nina vitu vingi nahitaji kufanya hasa kwenye jamii. Nahitaji kujihusisha sana na katika jamii ili project zangu zisaidie wengi,” alisema Lisa.
“Sitaki kusimamia mtu mmoja mmoja tena, kama hivyo watu kuwa chini ya menejimenti yangu,” aliongeza.
0 comments:
Post a Comment