,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Tuesday, December 29, 2015

Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe (Picha kutoka Maktaba)

DAR ES SALAAM
                                                                                                                
Siku chache baada ya kuteuliwa na Rais Wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli kuweza kuongoza Wizara ya Maliasili na Utalii. Waziri mwenye dhamana ya kuongoza wizara hiyo Profesa Jumanne Maghembe Ameanza kwenda na Kasi ya Magufuli inayotambulika Duniani kote kama "HAPA KAZI TU"

Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, amesema kipaumbele chake kikubwa kitakuwa ni kupambana na ujangili nchini.

“Niwaambie majangili sasa wakafanye kazi nyingine ama wakae nyumbani, kiama kinakuja huko, jambo la pili nitakaloshughulikia ni misitu, kuitunza na kupambana na usafirishaji wa magogo na ukataji wa mkaa,” alisema Profesa Maghembe.
Alisema kuwa atasimamia kwa uhakika maliasili za Watanzania kwa sababu mambo ya maliasili ndiyo eneo alilobobea kwenye usomi wake.

“Tutajitahidi pia kutangaza utalii na kuongeza mapato ya sekta hii kama tulivyofanya kwenye miaka ya 2006 hadi 2008, tuliongeza bei za vitalu na ada kwa mnyama mmoja mmoja anayewindwa,” alisema Profesa Maghembe.


0 comments:

Post a Comment

ufunguzi