SIMANZI! Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni (DC), Paul Makonda (pichani juu) amefunguka kuwa hakuna kitu asichopenda kukisikia kama watu wanavyodai kuwa wanawake wanaouza miili yao (machangudoa) na vibaka wanatokea wilayani kwake, jambo alilodai siyo sahihi.
Makonda alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akikabidhi vifaa vya michezo kwa makundi ya vijana wanaounda vikundi vya Jogging katika Viwanja wa Leaders Club jijini Dar.
Mimi siamini kabisa kwamba machangu na vibaka wanatoka Kinondoni, sasa hivi nataka ibadilike, vijana wajishughulishe na mambo mbalimbali na hii itawezekana, tena kwa kupitia vikundi hivi vya Jogging naamini tutaweza na huu ndiyo wakati wa kuamka,î alisema Makonda aliyekabidhi jezi na mipira ya soka na kikapu kama maandalizi ya Makonda Cup.
0 comments:
Post a Comment