Unapenda Selfie?
Vingi
vimesikika, wapo waliokamatwa kwa sababu walipiga selfie maeneo ambayo
hawaruhusiwi kufanya hivyo, hawa jamaa nao wamejikuta wakipoteza kibarua
baada ya kukiuka maadili ya kazi yao kwakujipiga selfie.
Ni
madaktari na manesi, walikuwa chumba cha operation Hospitali ya Shaanxi,
China wakiwa wanaendelea na jukumu lao basi ikatokea wazo la kupiga
selfie, wakati mgonjwa akiwa hana fahamu kalazwa akisubiri kufanyiwa
upasuaji. Kitendo cha kushare
picha hizo kwenye mitandao ya kijamii
kilipelekea madaktari na manesi kadhaa kfukuzwa kazi, huku wengine
watatu wakikabiliana na adhabu ya kukatwa mshahara wa miezi mitatu kila
mmoja.
Uongozi wa Hospitali hiyo umeomba radhi kwa
kitendo hicho, huku ukisema kuwa wafanyakazi hao walichukua picha hiyo
kama kumbukumbu ya siku yao ya mwisho kuwa kwenye chumba hicho kabla
hakijafungwa kwa ajili ya kufanyiwa matengenezo.
0 comments:
Post a Comment