Rais wa Poland Bronislaw Komorowsk amekubali kushindwa katika uchaguzi uliofanyika wiki iliyopita.
Hata hivyo matokeo rasmi hayajatolewa.
Matokeo ya awali yanaonyesha kwamba Komorowski ambaye ni mshirika wa serikali ya mrengo wa kulia, ameshindwa kwa asilimia 53 kwa asilimia arobain na saba dhidi ya mpinzani wake Andrzej Duda.
Matokeo haya hayakutarajiwa na Komorowski na yanachukuliwa kama tahadhari kwa serikali hasa wakati huu wa kuelekea uchaguzi wa wabunge baadaye mwaka huu.

0 comments:
Post a Comment