,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Tuesday, March 10, 2015

Mkurungezi mtendaji wa Mwanaharakati Mzalendo Media Krantz Mwantepele akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kufika katika kituo cha wazee wasiojiweza Msimbazi kinachosimamiwa na jimbo kuu hapa dar es salaam kanisa la katoliki na kuhudumia wazee wapatao kumi na moja waliokuwa wanaishi katika mazingira magumu.Timu nzima ya Mwanaharakati Mzalendo Media ilikuja hapa kuwaona wazee hawa na kupata nafasi ya kuwafariji na kutoa baadhi ya misaada ya chakula na nguo za kuwasitiri leo siku ya jumamosi tarehe 7/3/2015 
Mdau Marko Mlonganile akipata nafasi ya kumsalimia mmoja ya wazee wanaopatikana katika kituo hiki na kupata nafasi ya kujua baadhi ya changamoto zinazopatikana katika kituo hiki siku ya jumamosi tarehe 7/3/2015 
Mdau subilaga james akiwa katika taswira na mmoja bibi wanaopatikana katika kituo hiki cha wazee wasiojiweza kinachosimamiwa na jimbo kuu Dar es salaam la kanisa katoliki na kuweza kuhudumia wazee wapatao kumi na moja
siku ya jumamosi tarehe 7/3/2015 
Bibi ambaye ni mmoja ya wazee wanaotunzwa katika kituo hiki akitabasamu baada ya wadau wa Mwanaharakati Mzalendo Media kutembelea hapa na kuweza kuwafariji kwa kukaa nao na pia kutoa mahitaji kwa ajili ya chakula na nguo za kuwasitiri katika kituo cha wazee wasiojiweza hapa jijin dar es salaam kituo kinachosimamiwa na jimbo kuu Dar es salaam katoliki siku ya jumamosi tarehe 7/3/2015 

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi