,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Wednesday, March 11, 2015

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, akifungua Mkutano wa 59 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Hadhi ya Wanawake ( CSW), Mkutano huu wa wiki mbili ulioanza siku ya jumatatu, unafanyika ikiwa ni miaka 20 tangu kufanyika kwa mkutano wa kihistoria wa wanawake uliofanyika Beijing, China mwaka 1995. Mkutano huo uliokuwa chini ya Ukatibu Mkuu wa Dr. Gertrude Mongella, uliweka misingi mbalimbali iliyolenga katika kusimamia na kutetea haki mbalimbali za mwanamke zikiwamo za usawa wa kijinsia na uwezeshwaji.
Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akiwa na sehemu ya Ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mkutano wa 59 wa Kamisheni kuhusu Hadhi ya Wanawake ulioanza jana jumatatu hapa Umoja wa Mataifa
Sehemu wa washiriki wa mkutano wa 59 wa Kamisheni kuhusu Hadhi ya Wanawake wakifuatili hotuba za ufunguzi zilizotolewa na viongozi mbalimbali akiwamo Katibu Mkuu Ban Ki Moon na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Bw. Sam Kutessa

Na Mwandishi Maalum,  New York

Mkutano wa  59 wa Kamisheni  ya Umoja wa Mataifa kuhusu Hadhi ya Wanawake  maarufu kama  CSW umeanza rasmi siku ya jumatatu kwa hotuba  za ufunguzi kutoka kwa  viongozi mbalimbali akiwamo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon
Mkutano huu wa wiki mbili,   unafanyika  sambamba na  maadhimisho ya  miaka 20 tangu kufanyika  mwaka 1995  huko  Beijing , China, mkutano wa kihistoria  uliowakutanisha wanawake kutoka maeneo mbalimbali duniani.
Dr. Gertrude  Mongela,  ndiye aliyekuwa Katibu Mkuu wa mkutano huo wa Beijing,   uliotoka na  tamko lililoweka misingi  iliyolenga pamoja na  mambo mengine, kutetea na  kuimarisha hadhi  ya mwanamke,  usawa wa kijisia na  uwezeshwaji wa wanawake. 
Katika siku ya kwanza ya mkutano huo, wajumbe pamoja na kusikiliza hotuba za ufunguzi pia walipitisha kwa kauli moja,  Tamko la Kisiasa   linalosisitiza dhamira ya ya matokeo ya mkutano wa  kihistoria wa wanawake uliofanyika  Beijing mwaka  1995.

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi