,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Saturday, March 14, 2015

Na Victor Mariki – Ofisi ya Makamu wa Rais.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Binilith Mahenge ameishauri Halmashauri ya Jiji la Mbeya kutafuta wawekezaji watakaotumia taka kama malighafi katika shughuli uzalishaji viwandani ili kukabiliana na uchafuzi wa mazingira jijini humo.
Ushauri huo aliutoa, akiwa katika ziara ya siku mbili mkoani humo wakati alipotembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbeya na kuzungumza na Idara ya Usafishaji na Mazingira jiji humo jana.
Aliongeza kusema kuwa taka ni mali, zinaweza kutumika katika uzalishaji wa bidhaa nyingine huku akitolea mfano Kiwanda cha Falcon, kinachozalisha milango pamoja na chemba za vyoo kwa kutumia taka huko jijini Mwanza.
Pia katika ziara hiyo Mh. Mahenge, alitembelea Mtaa wa Ntungi, Kata ya Nsalaga ili kuona ujenzi wa dampo jipya lenye mita za ujazo 454,000, linaloweza kutumika ndani ya miaka sita ambalo ujenzi wake umewezeshwa na Benki ya Dunia kwa gharama ya shilingi bilioni 3.8.

Wakati huo huo pia, alitembelea hifadhi ya Safu ya Mlima Mbeya ili kujionea mikakati ya utunzaji mazingira inayotekelezwa katika hifadhi hiyo, ikiwemo upandaji miti kwa ajili ya kutunza vyanzo vya maji pamoja na ugawaji wa mbegu ya miti ya kuni bure kwa wananchi waishio karibu na hifadhi ili kuhepusha vitendo vya ukataji miti katika hifadhi hiyo.
Katika majumuisho ya ziara yake mkoani Mbeya, Mh. Mahenge alitembelea kiwanda cha saruji cha Mbeya Ciment, ambapo aliridhishwa na uendeshwaji wa shughuli za uzalishaji kiwandani hapo nakuupongeza uongozi wa kiwanda hicho kwa kuzingatia Kanuni za Mazingira.

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi