,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Thursday, February 26, 2015

Hakimu wa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, leo ametoa hukumu ya kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini kwa rapper, Chidi Benz.


Chidi alipandishwa kizimbani mahakamani hapo kusomewa mashtaka matatu ya kukutwa na madawa ya kulevya mwaka jana. Alikuwa nje kwa dhamana ya shilingi milioni 1 pamoja na wadhamini wawili wasiokuwa na hatia.

Faini anayotakiwa kulipa ni shilingi laki tisa. Chidi alikutwa na madawa ya kulevya aina ya heroin yenye thamani ya shilingi 38,638, na bangi yenye thamani ya shilingi 1,720 pamoja na na vifaa ya kuvutia dawa hizo ambavyo ni kijiko na kigae.

Tukio hilo lilitokea October 25 mwaka jana katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam akiwa anaelekea jijini Mbeya kwenye show.


Chanzo: bongo5

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi