sekondari mkoani Arusha
kupitia sanaa ya maigizo inayoelezea chimbuko la binadamu
imekuwa ikisaidia
kuongeza uelewa na mwamko wa wanafunzi kupenda masomo ya
sayansi.
Hayo yameelezwa na mkurugenzi wa Idara ya makumbusho ya
elimu viumbe ,mkoa wa Arusha, Felista
Mangalu, kwenye maonyesho ya sanaa ya sayansi ya chimbuko la
binadamu kwa shule
za sekondari yanayotolewa na kikundi cha sanaa cha
Scatterlkingis cha
Afrika kusini.
Mangalu,alisema kuwa ufundishaji wa sayansi kupitia
maonyesho ya sanaa ni mbinu mpya inayosaidia
wanafunzi kuyapenda zaidi masomo ya sayansi, na kutambua
kuwa sayansi ni ajira.
Alisema kuwa kikundi hicho kimeshatoa elimu hiyo kwa shule
kadhaa za sekopndari za
jijini Dar es Salaam, Karatu na Ngorongoro,ambapo wanafunzi
wamekuwa na mwamko
mkubwa wa kupenda masomo ya sayansi.
Amepongeza kuwa hii ni mara ya tatu kwa kikundi hicho cha
sanaa kutoka nchini afrika kusini
kufanya kufundisha sayansi kwa kutumia sanaa ya maigizo
,ambapo wanafunzi
wa sekondari kutoka shule mbalimbali za Arusha huwa
zinakusanyika makumbusho na kupata elimu hiyo.
Awali kiongozi wa kikundi hicho ,cha sanaa cha
Scatterlings,Profesa Robart Blumen Schine ,amesema kuwa
kupita sanaa wanafunzi wanaelewa chimbuko la binadamu na
mabadiliko yaliyotokea hadi kufikia kwenye sayansi na
teknolojia.
Alisema kuwa Tanzania inao utajiri mkubwa wa mambo ya
kale hasa
katika maeneo ya 0lduvai Georg na Laitory,na wanaendeleza
juhudi za kuelimisha
wanafunzi kupitia sanaa ili waweze kuelewa historia nzima ya
chimbuko la
binadamu kutoka hatua za mwanzo hadi kufikia ustaarabu.
Profesa,amesema kuwa kutumia sanaa wanfunzi wamekuwa na
mwamko mkubwa wa kupenda
sayansi na hivyo wanakuwa na uelewa wa hali ya juu wa
chimbuko la binadamu
Kwa upande wake Afisaa wa mpango wa elimu ya viumbe wa
makumbusho hiyo,Bura
Akonay, alisema kuwa binadamu tumebadilika kutoka hatua
mbalimbali
za mabadiliko ambayo yamewezesha binadamu kukabiliana na
mabadiliko hayo.
Amesema makumbushohiyo ni kitivo cha chimbuko la
mabadiliko ya binadamu kutoka enzi
ya zana butu za mawe hadi kufikia kutengeneza vifaa bora vya
kisasa kwa kutumia teknolojia.
Akonay,amesema njia hii ya kufundisha sayansi kwa kjutumia
sanaa inarahisisha na kuthibitisha
uwepo wa mabadiliko ya binadamu kutoka hatua moja kwenda
nyingine .
Ameongeza kuwa binadamu tumetoka asili moja na tumekuwa
tukibadilika kutoka hatua moja
hadi nyingine na hali hiyo inasababisha tuweze kuyakabili
mazingira yetu .
Ameongeza kuwa kusoma kwa kupitia sanaa kutasaidia kuwavutia
zaidi wananzi kusoma sayansi na kuwa
na kumbu kumbu nzuri ya chimbuko la binadamu.
0 comments:
Post a Comment