MSANII wa filamu, Wema Sepetu ambaye
anatarajiwa kuchapana makonde na Jacqueline Wolper katika pambano la
utangulizi kesho, amesema sasa amekwiva na yuko fiti kutokana na mazoezi
ambayo anapewa na kocha wake Rashidi Matumla.
Akizunguza na gazeti hili jana, Wema alisema ametumia muda mwingi katika mazoezi hivyo kesho ni lazima atampiga Wolper kwa ‘knock out’.
“Kwa kweli nimejifua vilivyo lengo likiwa ni kuhakikisha naweka historia kesho ya kumchakaza Wolper, kwa nilivyo fiti sidhani kama atafikisha raundi ya pili,” alisema Wema.
0 comments:
Post a Comment