Posted by Williammalecela.com on Thursday, August 31, 2017
 |
KOCHA Mkuu wa Yanga, Mzambia, George Lwandamina, amepatwa na msiba mzito baada ya baba yake mzazi kufariki.
Lwandamina ambaye amejiunga na Yanga Novemba, mwaka jana, amempoteza
baba yake huyo aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya kupooza ambapo
amefariki usiku wa Jumanne August 29, 2017.
Lwandamina amesema: “Kutokana na msiba huo, natarajia kuondoka leo
August 31 kwenda nyumbani Zambia kwa ajili ya mazishi na nikifika ndio
tutajua tunazika lini kwani nasubiriwa mimi tu nifike. “Baba
alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya kupooza na amefariki Jumanne usiku,
nikienda huko nitakaa mpaka kila kitu kimalizike na natarajia kurudi
Jumamosi ya wiki ijayo.” |
0 comments:
Post a Comment