Meneja
wa Diamond Platnumz, Sallam Sharaff amedai kuwa screen shots ya kile
kinachoonekana kuwa ni mazungumzo kati ya Wema na Diamond kupitia DM za
Instagram ni feki.
Katika mazungumzo hayo, Wema
anamueleza Diamond kuwa apuuzie kile mashabiki wake wanachokisema
kuhusiana na Zari na mtoto wao Tiffah na kwamba bado anampenda staa huyo
wa ‘Nana.’
Diamond naye anaonekana kupagawa na ujumbe huo na kumuomba waonane.
Hata hivyo Sallam Ambae ni Meneja wa Diamond kupitia Twitter amepuuzia screenshot hiyo kwa kudai kuwa ni feki.


0 comments:
Post a Comment