KUZALIWA MASKINI SI KOSA LAKO, LAKINI KUFA MASKINI NI KOSA LAKO MWENYEWE.
Je wewe umeajiriwa? Unalipwa kiasi gani kwa mwezi? Na je kiasi
unacholipwa kinatosha mahitaji yako na kutengeneza future yako? Kama
mshahara wako hautoshi unafanya lolote kuhakikisha unakuza kipato chako?
Hata kama umeajiriwa na unalipwa "mamilioni" kwa mwezi usibweteke..
tafuta fursa ya biashara fanya.. siku hizi hadi mawaziri wanafanya
ujasiriamali.. gavana wa BOT ni mjasiriamali mzuri tu. Sasa wewe
daktari wa "digrii" umeajiriwa Mwananyamala Hospital unalipwa tumilioni
tumoja unajiona umeula.. unaona wewe ni msomi na biashara ni za
waliofeli shule. Badili mtizamo otherwise utakufa maskini.
Na
kuna wale "kauka nikuvae" wanalipwa laki 5 kwa mwezi na wamebweteka tu
na kuridhika na hali za maisha yao.. Hivi unajua laki 5 kwa mwezi ni
sawa na Tsh 1,850 kwa saa? yaani dola moja. Ina maana umesoma mpaka chuo
kikuu halafu thamani ya lisaa lako moja ni dola moja tu!!!!?
Ndiyo maana watu wengi waliosoma sana huwa hawawezi kuwa matajiri kwa
sababu wanauza muda wao kwa "bei chee" halafu siku zinazidi kuyoyoma
haoni mafanikio. Huku tena ana mkopo wa gari nk. Makato na marejesho...
Kwa nini usife masikini kwa style hiyo.?
Shida ni kwamba watu
wanaabudu sana kuajiriwa na wako tayari watoe hata rushwa ya ngono (kwa
wadada) ili tu eti wajiriwe. Ajira imekuwa kama Mungu kwa wengine.
Wanafunzi vyuoni wanasubiri kwa hamu kumaliza shule ili wakaajiriwe
reception kupokea simu na kukaribisha wageni.. Seriously??
Halafu unasema umasikini unasababishwa na sijui na Richmond, mara sijui
Escrow.. Hivi unajitambua kweli.?? Halafu mnapost vikatuni vya #Shemeji_Unatuachaje? Hujui mtumaini cha shemeji hufa fukara!.
Sikia... maisha bora ni maamuzi yako binafsi. Hapo ulipo kuna watu
wanakuuzia vitu kila siku.. kuanzia dawa ya meno, sabuni, nguo za ndani,
suti unazovaa ofisini hadi chakula unachokula.. wewe unaona sifa tu
kila ukipita wanakuita "boss" kisa wanakuuzia kila kitu.. Umewahi
kujiuliza wewe unawauzia nini.??
Au ndo na wewe ndo umeamua
kuuza muda wako kwa bosi kwa kulipwa laki 5??. Halafu unashangaa baada
ya miaka 10 tangu uanze kazi bado unaishi nyunba ya kupanga.. huwezi
kusomesha watoto wako shule bora wala huwezi kusafiri ukapumzike na
familia Marekani, S.Africa au hata hapo Ngorongoro tu..
Bado
unakula ugali dagaa, wali njegere na bamia.. miaka 10 baada ya ajira..
siyo kwamba unapenda ila ni shida tu zinakulazimisha.
Sikiliza
nikuambie.. Dont sell your time in cheap way. You will die poor.
Utakaaje mwezi mzima unalipwa laki 5 na wewe ni graduate halafu
umeridhika eti "maisha ndo haya".. Acha ujinga.. Kama umeamua kuuza muda
wako basi let it be expensive. Ulipwe ghali.. na usiuze muda wote..
bakiza muda wa kukutosha kufanya ujasiriamali nje ya kazi.
Kuna
"vijitu" vinalipwa laki mbili na nusu kwa mwezi halafu vinatumia vocha
ya laki moja kuingia Facebook kumsifia Wema Sepetu ambaye hakujui hata
jina. Sijui #Team_Zari mara #Team_Wema.. yani ni ujinga ujinga tu.. Hivi Watoto wako watakula comment zako au? Au hiyo #Team_Wema na #Zari itakusaidia kulipia ada wanao??
Mbaya zaidi "wenye akili" tukiandika mambo haya vitatokea "vikaragosi"
vya kupinga na kutukana.. Na vingine wala havitasoma huu ujumbe.. na
vikisoma vitapuuza..
Wewe unayesoma hapa leo Chukua hatua ndugu!
Kumbuka maisha ni ya kwako na ni WEWE tu ndiye utakayeyabadili! Kila
siku kunapokucha jiulize umefanya nini kupiga hatua ya maisha yako
kutoka pale ulipokua jana. Jiulize maswali ya msingi na uchukue hatua.!
Change today. Usipobadilika utakufa maskini! Chukua hatua mpya ili upate matokeo mapya!
Acha wanaolalamika waendelee kulalamika. Bill Gates anasema: "KAMA
ULIZALIWA MASKINI SIYO KOSA LAKO, LAKINI KAMA UKIFA MASKINI HILO NI KOSA
LAKO"
Hakikisha unarudia kusoma ujumbe huu mara nyingi uwezavyo na hakikisha unashare na wengine.!
- Goodluckies Good, Mathew Jacob, Erick Mwakikato and 74 others like this.
- Ines Isaya akha sirudii ujumbe unachoooma..ila asante.
- Hendry-ki Da-voice Of course kuna fundisho kubwa sana #Malisa Godlisten
- Gift Macha Kaka umenigusa asilimia zote
- Baltazari Shayo Uko vizuri brow,tusibaki kupigia makofi mafisadi huku tunajikaanga na mafuta yetu wenyewe
- Ian Gisbert Asante sana mkuu
- Nelson Dickson tatizo mitaji na ufinyu wa connection, ukiajiriwa unaanza kujuhana na watu,then unachukua mkopo unafanya biashara zako...
- Paul Jacob Rohore Ujumbe uko poa sana na umeendana na wakati.Hongera kwa kuwatoa tongotongo vijana wenzangu kwani mimi pia ni mwanachuo nipo hapa IFM hayo yapo kweli kila unaemsikia kauli ni hizo hizo kutafuta temple au ajira akimiza.Utamsikia mtu eti nikipata sehemu nijiegeshe niwe napewa hata laki 2 tu nina uhakika wa kula.Yani mtu ana mawazo finyu kinoma.Mimi najituma nafight for future for better.One love.
- Paul Jacob Rohore Vijana tubadilikeni jamani tuache kulaumu kila siku vijiweni hakuna ajira hakuna ajira
- Idd Salum Naanza Kulima Bustan Na Kamshahara Kangu Ka Ualimu Haka! Bila Hvyo Nitakufa Njaa Haswa!
- Alala Shaidi Good new kaka
Ujumbe mzuri - Iññøcëñt Vìñçy Vînç Wale wa #team__upuuzi...change ur altitude...
- Mwalimu Ernest Mwakaluo Nalijua hilo toka mda ila umenikumbusha kitu.
- Ndabhizi Isumbicho WE..thubutu..nani arudie kusoma hii miiba......hapa tu ushanitoboa macho........then nirudie tena....au ni zhare na wengine....sahau...IMEINGIA Kiuraiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiini
- Kimwaga Junior Nakuaminia mkuu upo vzr saana!!
- Khamis Ramadhani Ahsante kwa ujumbe Bora, samahani sina maana ya kupinga lakini kuna wengine watachukua msitari mmoja tu unaosema"Acha wanaolalamika waendelee kulalamika "hawa watatumia mpaka muda wa mwajiri wake kufanya yake. Si vibaya kujituma narudia tena Ahsante.
- Saganda Saganda ni ukweli uliotukuka Malisa. kuwa masikin au tajili ni uamuzi wa mtu mwenyewe...
- Saganda Saganda Kingine Malisa kifupi pesa ziko kitaa yani mifukoni mwa watu zimejaaa ila sasa ni kazi yako kutengeneza networks ambazo zitaelekeza huo mtonyo mfukoni mwako...wasomi wengi hawana issue...kifupi wameikomboa elimu badala ya kuwakomboa wao...nakupata elimu cyo kazi kazi ni kuigeuza elimu uliyoipata kuwa pesa...
- Simon Gerald Asante ndugu japo "wabongo" wengi tunapendelea tu :confortable zone" ila mambo yanayoumiza akili kdg hatutaki lakin ndo wa kwanza kulalamikia ugum wa maisha ooh mara nchi imeuzwa wkt tunaona fahari kuvaa vitambulisho shingoni..vya waliotuajiri..halaf tunategemea muujiza flan
- Heladius Sabas Emmanuel Well said
- Wema Mrisho Mawazo mazuri asante
- Eustassy Salufu Get u Malisa
- Tatu Kajembe Ukifanya uku unapiga biashara maisha utayaona mazuri mno.ila kilichonichekesha kuliko vyote ni uteam wema na zari ha ha ha .mm mwnyw huwa nawashangaa sn mtu anatafuta vocha kwa ngv zote aingie.insta kumsifia wema eti amependeza kwny KTMA
- Daudi Gabriel Chukua mpe na ba Maggie Rose Kitojo
- Maro Masswe YAA.
- Rose Kitojo Mmmmmh haya ahsante sanaDaudi Gabriel Joseph J Lembule
- Tom Charles tnx brother
- Sadiki Tweve Kaka asante
- Nasir Kapinga Ushauri mzuri tena kwa watu sahihi tatizo wakati ulioleta huu ushauri nna mashaka nao Malisa Godlisten..Jamani ujasiriamali sio mchezo wa UPATU unahitaji umakini wa hali ya juu na ubunifu wa kiwango cha P.H.d..Ujasiriamali sio sehemu ya kupumzikia waun...See More
- Fredy Komu Nasir Kapinga umesema vyema.... juhudi na mtaji ni changamoto pia.... watu wengi hasa waliopo kwenye ajira wamekuwa watu wa kulaumu eti fulani ni mzembe kwa sababu hajishughulishi na biashara au ameanzishan biashara amehonga mtaji... Jamani hii haiitaji degree kujua kuwa.... biashara ya mtaji mdogo ina risk sana compare na ile ya mtaji mkubwa
- Faraja Simon ASANTE SANA KAKA Malisa Godlisten
- Buganda Bangili ujumbe mzuri sana
- Gasto Kessy Hii makala mkuu nielimu tosha mkuu ahsante kwa kutukumbusha safar ya maisha bora.
- Joseph Peter Sure u have constractive ideas daaaaah nimepata changamoto kupitia ujumbe wako unaojenga big up sana tumefanya kazi pamoja SAUT ila nilikuwa cjukujui vizur unamawazo mazuri kiac hiki kamanda Malisa Godlisten


































0 comments:
Post a Comment