TANZANIA NCHI YA KUSADIKIKA.?
By Malisa GJ,
Tanzania bhana.. hii nchi ina vituko vyake very unique. Tunaishi kama
nchi ya kusadikika vile... Eti wakubwa flani walikaa wakaona njia ya
kupunguza foleni Dar ni kununua boti ya kwenda Bagamoyo. Itasaidia
kupunguza msongamano New Bagamoyo Road kwa waendao Mbezi Beach, Tegeta,
Bokko na pia wasafiri wa Bagamoyo watafika haraka.
Boti ikanunuliwa. Nimeiobserve pale Ferry inatumia masaa mawili na nusu
kufika Bagamoyo kutokea Dar and itz vice versa; while kwa bus ni one
hour na kwa self drive ni less than an hour. Last week nimetumia nusu
saa kudrive Dar to Bagamoyo na nusu saa kurudi. Tafsiri yake ni
kwamba ukiwa na gari binafsi unaweza kwenda Bagamoyo na kurudi mara 5
ndio Boti ifike. Ina speed ndogo kuliko trekta.
Sasa baada ya
serikali kuona "gia" ya mwendokasi imefeli, wamekuja na mpya nyingine.
Waziri wa Uchukuzi akijibu hoja bungeni amesema lengo la kununua boti
sio usafiri wa haraka tu bali pia ni "adventure na starehe" kwa
wasafiri.
Hivi kweli Bagamoyo Dar ni adventure? Kama mtu anataka
adventure si apande pantoni ya Mv.Magogoni ashinde huko siku nzima bila
kushuka.. Hata hivyo je hiyo boti ina mazingira ya kuenjoy na
kufanya adventures? Boti watu wanapanda na kuku, samaki, pweza, ngisi,
nazi, na mananasi ndio adventure?
Boti inazidiwa mbali mno na
Kilimanjaro IV ya Bakhresa. Bora hata watu wapande Kilimanjaro IV
wanaweza kupata adventure sio hiyo boti ya serikali ambayo inaweza
kuzima anytime katikati ya maji. Boti ya Bakhresa inatumia
dakika 90 kutoka Dar hadi Zanzibar, boti ya serikali inatumia masaa
mawili na nusu kufika Bagamoyo afu tunaambiwa ni adventure. Hivi hii
ikienda Zanzibar si itatumia wiki nzima?
Sasa naanza kumuelewa Mkosamali aliposema ukitaka matatizo nchi hii tumia vitu vya serikali. Yani ni aibu.. Mtanzania hana ajira, hana hela ya kula, hana ada ya kulipia wanae
shule, hana kodi ya nyunba, halafu eti unamletea boti ya kufanya
adventure? Hivi serikali ya CCM huwa inafikiria kabla ya kufanya
maamuzi??
Halafu kichekesho nasikia imenunuliwa "ghali" zaidi
kuliko Kilimanjaro IV ya Bakhresa.! Eeh Mungu tunusuru na janga la CCM.
Malisa GJ.!

0 comments:
Post a Comment