KUJISHUSHA! Staa wa filamu Bongo, William Mtitu amesema yupo tayari kumaliza ugomvi na Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ kutokana na shinikizo kutoka kwa wasanii wenzake, wadau na mkewe.
Kwa mujibu wa chanzo makini, kikao kizito kikimhusisha Mtitu na wasanii nguli kiliitishwa na kumuonya juu ya suala hilo kabla ya kukubali kuwa yuko tayari kumalizana na Steve.
Mwandishi wetu alimtafuta Mtitu ili kusikia chochote kutoka kwake ambapo alisema;
“Duh! Umeipata na hiyo! Ni kweli kabisa, hakuna haja ya kuwa na mabifu katika zama hizi za maisha mafupi, wakiandaa mpango wa kutukutanisha, niko tayari.”
Kwa upande wake, Steve Nyerere alisema asingeweza kulizungumzia suala hilo kwa wakati huo kwani alikuwa na kazi anaifanya. Aliahidi kumtafuta mwandishi baadaye, lakini hadi Risasi Mchanganyiko linakwenda mitamboni, alikuwa hajawasiliana naye.
0 comments:
Post a Comment