Serikali ya Kenya imeahidi
kuwasamehe wakenya ambao wamepokea mafunzo ya kigaidi endapo
watajitokeza katika kipindi cha siku 10 zijazo.
Waziri wa usalama wa ndani jenerali mstaafu Joseph Nkaissery pia amewaonya wazazi wa vijana kama hao kwamba watachukuliwa hatua kali endapo hawataijulisha serikali kuhusu kujiunga kwa wanao na kundi la Al Shabaab.
Serikali imewapa wale wote waliopokea mafunzo kutoka kwa Al Shabaab siku kumi kupiga ripoti kwa afisi za wasimamizi wa miji ya Garissa, Mombasa ama Nairobi.
Hofu imeibuka nchini Kenya baada ya ripoti kwamba mmoja wa wanamgambo walioshambulia chuo kikuu cha Garissa na kuchangia kuwaua watu 147 alikuwa Mkenya aliyesomea taaluma ya sheria jijini Nairobi. Babake, ambaye ni chifu, alipiga ripoti kwa serikali alipotoweka mwanawe miaka miwili iliyopita.
BBC

0 comments:
Post a Comment