Mwandishi mpiga picha wa ITV, Hussein Nuha (30) akiwa katika wodi ya daraja la kwanza akiugulia maumizi baada ya kupata ajali eneo la barabara kuu ya Dar es Salaam kwa kuligonga basi la Happy Afrika lililokuwa likitokea Njimbe kwenda Dar es Salaam baada ya kuingilia msafara wa mkuu wa mkoa wa Morogoro na kulazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro kabla ya kuhamishiwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi kwa upande wa kichwa jana.PICHA/MTANDA BLOG.
Mwandishi wa gazeti la Mtanzania mkoa wa Morogoro, Kuty Libenanga kulia akisaidia huduma ya kwanza kwa mwandishi mpiga picha wa ITV, Hussein Nuha wakati akifikishwa hospitalini hapo.

MEYA WA MANISPAA YA MOROGORO:
Meya wa Manispaa ya Morogoro Amir Juma Nondo akiwa katika wodi ya daraja la kwanza hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro baada ya kupata ajali na waandishi wawili na dereva wake ambapo walijeruhiwa vibaya.
Dereva wa gari la Meya wa Manispaa ya Morogoro, Ally Mwambara akiwa katika kitanda cha wagonjwa akielekea wodini kulazwa baada ya kupata ajali eneo la Mizambarauni kwa kugongana na basi la Happy Africa lililokuwa likitokea Njombe kuelekea Dar es Salaam katika barabara kuu ya Dar es Salaam-Morogoro wakati wakitoka katika ziara ya mkuu wa mkoa wa Morogoro jana.
0 comments:
Post a Comment