Posted by Williammalecela.com on Tuesday, November 25, 2014
 |
SINEMA YA "ESCROW"
Naiona sinema inayoendelea juu ya Escrow..
Wakati Zitto akisema ripoti imejaa madudu mengi na wakubwa wengi
wameshiriki, Mama Tibaijuka nae anaibuka na episode mpya ya kumshutumu
Zitto kulipiwa kesi yake na PAP.
Wakati Ndugai anasema hakuna
kesi yoyote iliyopo mahakamani hivyo bunge litajadili kama kawaida,
Makinda anasema kuna kesi Polisi na anazuia mijadala.
Wakati Nape anasema kila mtu atabeba msalaba wake Pinda anasema hakuna
wa kubeba msalaba maana ripoti ya Escrow ni safi na haijamhukumu yeyote
(soma Majira ya leo).
Wakati TAKUKURU wakisema Pesa zilizochotwa
na PAP ni za Umma inadaiwa ripoti ya CAG imewasafisha PAP na kudai ni
hela yao halali baada ya kushinda offer ya IPTL dhidi ya TANESCO, na
kwamba BOT walikua watunzaji tu but sio hela yetu.
Duuuh.! Nasikia kiu... Sijui "episode" inayofuata saivi itakuwaje maana hii movie ya ESCROW ni kali kweli.
|
0 comments:
Post a Comment