,./.,

,,

... ...

';';';';

''=

==

adv
Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Sunday, June 16, 2013

Uchaguzi wa Madiwani wa Kata nne za Jiji la Arusha uliokua ufanyike leo umeairishwa hadi tarehe 30/06/2013 mwaka huu,uchaguzi huo umeahirishwa kufuatia shambulio la kigaidi lililotokea jana katika Mkutano wa kufunga kampeni ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Akizungumza na Habarimpya.com jijini Arusha Mkurugenzi wa Jiji hilo Sipora Liana amesema uchaguzi huo umeairishwa kutokana na sababu za Kiusalama,na kwamba utafanyika katika tarehe hiyo endapo hali itatulia.
"Tumelazimika kuahirisha uchaguzi huo kwa sababu za kiusalama, hatuwezi kuendelea na uchaguzi katika hali kama hii, hali si shwari katika Jiji la Arusha na hata tarehe hiyo iliyopangwa pia inaweza ikaahirishwa endapo hali haitakuwa shwari"alisema Liana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema katika tukio hilo watu wawili mwanamke na mwanamume wamepoteza maisha, huku akidai kwamba bado wanafuatlia idadi ya majeruhi waliotawanywa katika Hospitali mbalimbali  mkoani humo.
Hilo ni tukio la pili la bomu kulipuka katika mkusanyiko wa watu wengi mkoani humo, Mei 5 mwaka huu bomu lililipuka katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasit mjini Arusha na kuua watu watatu na wengine kujeruhiwa.

0 comments:

Post a Comment

ufunguzi