Taarifa Muhimu Kwa Umma Kutoka Benki Kuu ya Tanzania
Benki Kuu inapenda kuutahadharisha umma kuwa katika siku za
karibuni kumekuwepo na mtandao wa matapeli unaotumia TOVUTI ifuatayo www.jakayafoundation. wapka.mobi/index.html
. Mtandao huo unajidai kuwa ni Taasisi ya Fedha ijulikanayo kwa jina la
Jakaya foundation ambayoinamilikiwa na Benki Kuu chini ya utawala wa
bodi kuu ya mikopo inayotolewa na serikali kupitia sekretariat ya
Utumishi wa umma ofisi ya Rais.
Matapeli hao wanaeleza kwamba Taasisi hiyo inatoa mikopo ndani ya
masaa 24 kwa Mtanzania yeyotemwenye umri kuanzia miaka 18 endapo
atajiunga kwa kulip a ada ya shilingi 37,000/=.BENKI KUU INAUARIFU UMMA
KUWA HAIITAMBUI NA WALA HAIHUSIANI KWA NAMNA YOYOTE ILE NA TAASISI
INAYOELEZWA KWENYE TOVUTI HIYO.
Kwa taarifa hii, Benki Kuu inatoa tahadhari kwa Wananchi
kutojihusisha na Taasisi hiyo ya kitapeli kwa ajili ya kupata huduma za
mikopo kama ambavyo inadai.
IMETOLEWA NA IDARA YA UHUSIANO NA ITIFAKI BENKI KUU YA TANZANIA DAR ES SALAAM. 29/5/2013
0 comments:
Post a Comment