Edgar Mwandeman
- TANGAZO
MKUTANO WA WANACHUO WOTE
Jumuiya ya Wanafunzi Vyuo Vikuu wanaotokea Kyela inawatangazia wanavyuo wote walioko Kyela wakati huu wa likizo kuwa, kutakuwa na mkutano wa Wanavyuo wote walioko Kyela.
Mkutano huo utafanyika Jumamosi tarehe 7.06.2012 kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 7:00 mchana katika ukumbi wa KBC-Kyela Fm (Ukumbi wa Super Market).
Lengo la mkutano huo ni kufahamiana miongoni mwa wanavyuo, kujiwekea mikakati ya namna ya kusaidiana na jamii yetu kutatua changamoto mbalimbali za kimaendeleo, na kuandaa namna vyuo vingine vinavyoweza kuanzisha matawi ya Jumuiya.
Tafadhali usikose kuhudhuria Mkutano huu muhimu.
Tangazo hili limekujia kwa hisani ya Kyela Fm Community Radio na Jumuiya ya Wanafunzi Vyuo Vikuu.
Limetolewa na:
Katibu Mkuu wa Jumuiya
Kwa mawasiliano zaidi piga: 0756 783 963 (Mwenyekiti); 0769 981 357 au fika moja kwa moja kwenye ofisi za Kyela Fm Community Radio fm (96.0)
0 comments:
Post a Comment